• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
TUNDUMA TOWN COUNCIL
TUNDUMA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MJI TUNDUMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mipango
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Divisheni ya Miundombinu na Maendeleo ya Miji na Vijijini
      • Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
  • Fursa na Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya , Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Lishe bora kwa Afya imara
      • Mapambano dhidi ya Malaria
      • Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya
      • Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI
    • Huduma ya Elimu
      • Huduma ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi
      • Huduma ya Elimu ya Sekondari
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya Kilimo
    • Huduma ya Mifugo
    • Huduma ya Uvuvi
    • Huduma ya Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Uchumi, Mipango Takwimu
      • Kamati ya Elimu, Afya na maji
      • Kamati ya Kazi, Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Ethics Committee
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Instagram
    • Facebook
  • Nyaraka
    • Nyaraka
    • Miongozo

MAKAMU WA RAIS MHE. DKT. PHILP MPANGO AFUNGUA MAONYESHO YA NANENANE 2023 MBEYA

Imewekwa : August 1st, 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amekemea tabia ya uvamizi na mtindo wa kubadili matumizi ya ardhi iliyotengwa mahsusi kwa ajili ya Utafiti wa Kilimo.

Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo leo tarehe 01 Agosti 2023 wakati akifungua maonesho ya Nane nane kitaifa yanayofanyika katika viwanja vya John Mwakangale mkoani Mbeya. Amesema maeneo mengi ya taasisi za utafiti yamevamiwa na kupimwa viwanja jambo ambalo linatishia utafiti wa kilimo na mifugo kwa kuwa vituo vya utafiti vitakosa maeneo ya kutosha ya kufanyia kazi.

Makamu wa Rais amewataka watanzania kutambua kilimo ni sayansi na hivyo utafiti kilimo usipopewa kipaumbele basi mapinduzi ya kilimo yatabaki kuwa ndoto. Amesisitiza umuhimu wa kupima maeneo ya taasisi za utafiti wa kilimo, kupewa hati na kulindwa wakati wote. Vivyo hivyo ameelekeza mamlaka zinazohusika kutenga na kupima ardhi katika maeneo ya uzalishaji wa mbegu na kuyalinda dhidi ya uvamizi.

Vilevile Makamu wa Rais amekemea uwepo wa makundi makubwa ya mifugo yalioingizwa katika mikoa ya nyanda za juu kusini. Amesema madhara yake ni makubwa ikiwemo kuharibiwa sana kwa mazingira kuongezeka kwa migororo mingi kati ya wakulima na wafugaji, wanyama kama Tembo kukimbia bugudha ya mifugo na kuhamia kwenye makazi ya binadamu wakiharibu mazao na hata kuua watu. Amezitaka Wizara zote husika na Wakuu wa Mikoa kuchukua hatua thabiti kudhibiti uingizaji mifugo kinyemela katika maeneo yao ya utawala.

Makamu wa Rais ametoa wito kwa wakulima, wafugaji na wavuvi kuzingatia maelekezo ya wataalam ili kuweza kuzalisha pasipo kuathiri afya ya binadamu na mazingira kutokana na kuongezeka kwa matumizi yasiyo sahihi ya viuatilifu na kemikali nyingine jambo lenye athari kubwa kwa afya ya binadamu na viumbe hai vingine.

Ameongeza kwamba Serikali inaendelea kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji nchini ikiwemo kujenga mabwawa ya kuvuna maji ya mvua kwa ajili ya umwagiliaji, ambapo lengo ni kufikia eneo la umwagiliaji la hekta 1,200,000 ifikapo mwaka 2025. Pia ametoa wito kwa wananchi kutumia na kutunza miundombinu hiyo ili iweze kutumika kwa muda mrefu na kusaidia kuleta tija.

Makamu wa Rais ametoa rai kwa wakulima kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula ili taifa liweze kujitosheleza kwa chakula na kupata fedha zaidi za kigeni kutokana na mazao mbalimbali. Amasema Serikali kwa upande wake itaendelea kuimarisha utoaji wa huduma za ugani kwa kuwapatia Maafisa Ugani vitendea kazi mbalimbali vikiwemo pikipiki, vifaa vya matibabu, uhimilishaji pamoja na vifaa vya kupima afya ya udongo.

Ameitaka Wizara ya Kilimo na Mifugo kuanza maandalizi ya kuchukua vijana wengine katika programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (Building a Better Tomorrow - BBT) pamoja na kuziagiza Wizara za Kilimo na Mifugo na Uvuvi kuona namna bora ya kushirikiana na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ili vijana wa JKT wanaojitolea wapewe kipaumbele kushiriki katika programu hiyo.

Makamu wa Rais ameendelea kusisitiza taasisi za fedha na mabenki hapa nchini kuendelea kushusha riba zaidi ili kuwasaidia wakulima na wafugaji. Ameitaka Wizara ya Kilimo na Fedha kufikiria kuanzishwa kwa mfuko wa maendeleo ya kilimo utakaosaidia kushusha riba kwa wakulima, wafugaji na wavuvi.

Amewapongeza watafiti waliosaidia katika upatikanaji wa mbegu na kutoa wito kwa Wizara ya Kilimo kutafuta utaratibu wa kuwapa tuzo vijana na wabunifu wanaotoa suluhu ya mambo mbalimbali katika kilimo, ufugaji na uvuvi.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema sekta ya kilimo inaendelea kuimarika kutokana na juhudi za serikali katika kuinua sekta hiyo ikiwemo kuongezeka kwa bajeti kufikia shilingi bilioni 970 kutoka bilioni 294. Ameongeza kwamba kuimarika kwa sekta hiyo kumepelekea kuzalishwa kwa kahawa tani 80000, tumbaku kilo milioni 120 huku uzalishaji wa pamba ukiongezeka mara mbili. Bashe ameishukuru serikali kwa kutoa shilingi bilioni 100 ili kusaidia makampuni ya pamba yaweze kununua zao hilo kwa wakulima.

Waziri Bashe amesema maendeleo ya kilimo yanategemea ufanisi katika sekta zingine ikiwemo bandari. Ameongeza kwamba mabadiliko na uwekezaji wa tija katika bandari yanahitajika kwa sasa kwani yatasaidia wakulima katika kusafirisha mazao yao.

Pia amesema kuanzia mwaka 2024 nchi zote za Afrika zitapata mialiko ya kuhudhuria maonesho ya Nane nane huku akisisitiza mialiko hiyo haitahusisha viongozi pekee bali hadi wakulima na wanunuzi wa mazao wa nchi hizo. Ameongeza kwamba kufuatia kupanda hadhi kwa maonesho hayo kuwa ya kimataifa, juhudi mbalimbali zinaendelea ikiwemo kuboresha maeneo yanayotumika kwa ajili ya sherehe hizo kwa kuyajenga ili yawe ya kudumu.

Matangazo

  • Tangazo la Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 May 14, 2025
  • Orodha ya Majimbo Mapya na Yaliyobadilishwa Majina May 12, 2025
  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Watahiniwa 694 Kufanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 2025 May 03, 2025
  • Taarifa kwa Umma February 27, 2025
  • Onyesha Zote

Habari mpya

  • Mei Mosi Songwe Yafana

    May 01, 2025
  • Chaurembo Awapongeza Walimu

    April 30, 2025
  • Tunduma kwa Taaluma Sina Mashaka Nanyi: RAS Seneda

    April 30, 2025
  • Chaurembo Afungua Mafunzo Uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Pili

    April 29, 2025
  • Onyesha Zote

Maktaba ya video

Ubunifu mkoa wa Songwe
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Songwe Shindani Blogspot
  • Watumishi Portal
  • Tunduma yapata hati Inayoridhisha
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2019
  • Tangazo la kazi sekta ya Afya
  • Sherehe za Muungano
  • Kibali cha Matangazo

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais, Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti ya Mkoa wa Songwe
  • OR-TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Msampania, Chapwa - Tunduma

    Sanduku la Posta: P. O. BOX 73

    Simu ya Mezani: +255 25 2957388

    Simu ya Mkononi: +255 756 427 307

    Barua Pepe: td@tundumatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya mji Tunduma. Haki zote zimehifadhiwa